Monday 16 May 2016

WALIOTAPELI SH 62 BILIONI UINGEREZA WASAKWA DAR…

Shirika la Kimataifa la Polisi linawasaka raia wawili wa Scotland, wanaodaiwa kukimbilia Tanzania
baada ya kufanya udanganyifu na kujipatia Paundi 20 milioni za Uingereza (sawa na Sh62 bilioni).

Wawili hao Gareth Johnson (48) na Geoffrey Johnson (72) walikuwa sehemu ya kundi la watu 18, lililohusishwa na uhalifu huo wa uchakachuaji ongezeko la kodi ya simu za mkononi nchini Uingereza.
Kutokana na kosa hilo Mahakama Maalumu ya Mapato na Forodha ya Uingereza (HMRC), iliamuru wanafamilia hao ambao ni baba na mwanae, walipe fidia ya Paundi 109 milioni (sawa na Sh337 bilioni).
Lakini hukumu hiyo ilitoka bila ya wawili hao kuwapo baada ya kutoroka kabla ya shauri hilo kuanza kusikilizwa na inasemekana walikimbilia Tanzania.
Akizumgumzia suala hilo Mkuu wa Interpol Tanzania Gustavus Babile, amesema kibali cha kimataifa cha kukamatwa kwa wawili hao kipo kwenye tovuti yao.
Amesema walipokea taarifa kutoka Uingereza hivyo hatua inayofuata ni kukipeleka kibali hicho mahakamani kwa ajili kupata nguvu za kisheria za nchi.

Hadi sasa inadaiwa kuwa Geoffrey na kijana wake wamekuwa mafichoni Tanzania kwa takriban miaka mitatu sasa.

0 comments:

Post a Comment