Monday 2 May 2016

WANAJESHI WA UINGEREZA WAWASILI SOMALIA…!!

Kikosi kidogo cha jeshi la Uingereza kimewasili nchini Somalia kusaidia wanajeshi wa muungano
wa Afrika walioko huko.

Karibu wanajeshi 10 wa uingereza watafutiwa na kikosi kingine cha wanajeshi 70.
Watasaidia kutoa huduma za matibabu, usafiri na za kiufundi.

Waziri wa ulinzi wa Uingereza Michael Fallon anasema kuwa kikosi hicho kitasaidia kuleta udhabiti na kukabiliana na tisho kutoka kwa wanamgambo nchini Somalia.

0 comments:

Post a Comment