Friday 6 May 2016

MADAKTARI WAPANDIKIZA VIUNGO VYA WENYE UKIMWI..!

Madaktari nchini Uingereza wamefanikiwa kwa mara ya kwanza kupandikiza viungo vya watu wanaougua Ukimwi kwenye wagonjwa wanaougua Ukimwi.

Kwa jumla, figo mbili na maini mawili vilipandikizwa kwa watu waliokuwa wameathirika sana na Ukimwi.
Viungo vilitolewa kwa watu baada yao kufariki.
Wataaamu wanasema mafanikio hayo yatasaidia kupunguza uhaba wa watu wanaoweza kutoa viungo na wanatumai kwamba watu zaidi wanaougua Ukimwi watajitokeza kutoa viungo vyao.
Kwa jumla, nchini Uingereza, watu watatu hufariki kila siku wakisubiri kupata viungo vya kupandikiziwa.
Ingawa kwa sasa viungo vya watu wenye Ukimwi vinaweza tu kutolewa kwa watu wanaougua Ukimwi, mtaalamu wa upandikizaji Prof John Forsythe anasema hilo bado litasaidia kwa sababu litawezesha kufanyika kwa upandikizaji katika hali ambazo awali haingewezekana.

Upandikizaji wa kwanza wa figo kwa watu wanaougua Ukimwi ulifanyika katika hospitali za Guy na St Thomas' Hospital jijini London mwaka 2015.

0 comments:

Post a Comment