Tuesday 10 May 2016

JAJI ASEMA UBAKAJI NI KAWAIDA KWA WANAUME WA AFRICA....!!

Jaji mmoja mzungu nchini Afrika Kusini ameshutumiwa vikali, baada ya kudaiwa kusema kwenye mitandao ya kijamii kwamba ubakaji ni kawaida kwa wanaume weusi.

Jaji Mabel Jansen alisema unajisi wa watoto na wasichana na pia ubakaji wa wanawake, ni jambo la kufurahiwa la kupitisha miongoni mwa Waafrika.
Kadhalika amenukuliwa pia akisema hajawahi kukutana na msichana mweusi ambaye hajawahi kubakwa.
Akijitetea jaji huyo amesema amefasiriwa vibaya na kwamba matamshi hayo yametumiwa vibaya nje ya muktadha.
Jaji Jansen anadaiwa kutoa matamshi hayo kwenye mawasiliano na mwanaharakati Gillian Schutte kwenye Facebook mwaka jana lakini yamesambazwa sana wikendi.
Wakili mashuhuri Afrika Kusini Vuyani Ngalwana amesema kuwa, matamshi hayo ya jaji huyo yanawaharibia sifa wanaume wote weusi na kuwaonesha kama wabakaji.
Amesema ni maneo ya kushangaza sana kwa mujibu wa gazeti la Business Day.
Kampeni imeanzishwa nchini humo ya kutaka jaji huyo afutwe kazi.
Bw Ngalwana amesema Tume ya Huduma za Mahakama inafaa kumtaka afafanue matamshi hayo kabla ya kumchukulia hatua.
Msemaji wa chama tawala cha African National Congress (ANC), amesema anashuku kuna majaji wengi wenye mtazamo wa kibaguzi.

Utawala wa Wazungu ambao ulihalalisha ubaguzi wa rangi, ulifikia kikomo nchini Afrika Kusini mwaka 1994.

0 comments:

Post a Comment