Thursday 23 June 2016

ITALIA YAWATAKA WATENGENEZA PIZZA KUSOMA ZAIDI…..

Kundi la maseneta wa Italia wametoa wito kwa watengenezaji wa Pizza nchini humo, kupasi mitihani yao ili kuboresha viwango vya uandaaji wa mlo huo.

Wabunge 22 katika bunge la juu wamewasilisha mswada bungeni ambao ukipitishwa kuwa sheria, itapendekeza kusajiliwa kwa taaluma maalum ya pizzaoli (wapishi wa pizza)
Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na shirika la habari la Rai,Taaluma hiyo itajumuisha kozi zitakazosomewa kwa jumla ya saa mia moja ishirini, itakayomuezesha mwanafunzi kufuzu ngazi ya Diploma.
Katika mapendekezo hayo wale wanaopania kuwa Pizzaoli, wanastahili kupasi mtihani wa nadharia na wa vitendo, baada ya kusomea sayansi ya chakula,usafi na lugha za kigeni msisitizo zaidi ukipewa lugha ya kiingereza.
Wale ambao wamekuwa wakitengeza pizza kwa angalau miaka kumi au zaidi,ambao wanaweza kuungana katika kikundi cha watu wanne moja kwa moja watatambuliwa kama "master Pizzaoli"
Maseneta hao wanasema karibu pizza milioni nne huliwa kila siku Nchini Italia, hivyo ipo haja ya kuandaa pizza inayofikia viwango vya juu.
Italia ina jukumu la kudumisha hadhi yake kwa kuwa inafahamika kwa uandaaji wa pizza za aina yake duniani.


0 comments:

Post a Comment