Picha za watu wa kada mbalimbali nchini wakiigiza ‘staili’ mpya ya
wabunge wa
Ukawa waliojibandika karatasi midomoni zenye ujumbe tofauti kuhusu
haki ya uhuru wa Bunge wanayodai kuminywa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson
zimeiteka mitandao ya kijamii nchini.
Tukio la wabunge hao lilitokea juzi
mjini Dodoma ikiwa ni mwendelezo wa siku 17 za kususa vikao vinavyoongozwa na
Dk Tulia tangu akatae kujadili hoja ya kusimamishwa wanafunzi 7,802 wa
stashahada maalumu ya sayansi katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), wiki tatu
zilizopita.
Kama ilivyokuwa kwa wabunge hao watu
mbalimbali wanapiga picha za kuigiza tukio hilo na kuziweka katika mitandao ya
facebook, twitter na Instagram, baadhi wakiandika ujumbe kwenye karatasi
wanazobandika midomoni ama wakiwaponda Ukawa au wakiwaunga mkono.
Mbali na waliobandika karatasi
midomoni, wengine waliamua kujiziba kwa nguo, vilemba huku baadhi wakitumia
kadi za CCM na Chadema na kuweka ujumbe wa kukosoa au kupongeza tukio hilo huku
wengine wakitumia neno ‘kuziba mdomo’ kutoa yao ya moyoni ambayo hayahusiani na
kitendo cha wabunge wa Ukawa.
Tukio hilo lilivuta wafuatiliaji wengi katika mitandao hiyo, katika
ukurasa wa facebook wa gazeti la mwananchiNews, watu 255,372 walifungua picha
za wabunge hao wa Ukawa huku watu 922 wakizinakili na kuzituma katika kurasa
zao za mtandao.
0 comments:
Post a Comment