Tuesday 24 January 2017

CHAGUO LA MAKAMU WA URAIS LAZUA UTATA GAMBIA...!

Rais mpya wa Gambia Adama Barrow amemteua mwanamke mwenye ushawishi mkubwa, ambaye aliwahi kuwa mshirika wa aliyekuwa rais wa taifa hilo Yahya Jammeh kabla ya kujiunga na upinzani ulioshinda uchaguzi kuwa makamu wake wa urais.

Aidha mwanamke huyo kwa jina Fatoumata Jallow-Tambajang alimtishia kiongozi huyo kwa kumfungulia mashtaka.
Lakini watu wanatilia shaka iwapo bi Tambajang mwenye umri wa miaka 68 anahitimu kupewa wadhfa huo kutokana na umri wake.
Bi Tambajang aliwahi kuhudumu kama waziri wa afya na maswala ya kijamii wakati wa utawala wa Yahya Jammeh lakini akalazimika kwenda mafichoni baada ya kukosana naye.

Baadaye alikuwa kiungo muhimu katika kuanzisha upinzani uliomshinda Jammeh mnamo tarehe mosi mwezi Disemba, na alikuwa wa kwanza kumtishia kwamba atamfunguliwa mashtaka kwa uhalifu aliotekeleza wakati wa utawala wake,wito unaoenda kinyume na rais Adama Barrow.

0 comments:

Post a Comment