Monday 30 January 2017

HAKIMU MMOJA ASIKILIZA MASHAURI 400 KWA MWEZI....

Imeelezwa kuwa uhaba wa mahakimu katika Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi imefanya kila hakimu katika mahakama hiyo kuwa na mzigo wa mashauri 400 kwa mwezi mmoja.
kufuatia hali hiyo, mahakama imeomba Mabaraza za Ardhi ya Vijiji, Kata, na ya Nyumba ya Wilaya kuondolewa katika ngazi ya utoaji hukumu na usuluhishi wa kesi za migogoro ya ardhi nchini ili kusaidia kuharakisha utatuzi wa migogoro ya ardhi
Akizungumza na Hot Mix leo katika maonesho ya wiki ya sheria yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam, Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, Frank Mahimbali ambaye amesema, kuwepo kwa vyombo vingi vya usuluhishi na maamuzi katika utatuzi wa migogoro ya ardhi nchini kunachangia ucheleweshwaji wa kusikiliza mashauri ya migogoro ya adhi.
Amesema, ni vyema shughuli za utatuzi wa migogoro ya ardhi ikaachiwa Mahakama pekee kutokana na maamuzi mengine yanayofanywa na ngazi hizo kuwana mgongano wa kimaslahi baina ya wizara na taasisi zinazosimamiwa na ngazi hizo na kuchangia ucheleweshwaji wa kesi.

Aidha Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi Frank Mahimbali, ameeleza kuwa kwa sasa Mahakama Kuu ya Divisheni ya Ardhi ina mahakimu wa 5 pekee huku idadi ya mashauri ikiwa ni 2,217 jambo linalopelekea hakimu mmoja kusikiliza mashauri 400 kwa mwezi hivyo kuiomba serikali kuongeza mahakimu katika mahakama hiyo.

0 comments:

Post a Comment