Monday 30 January 2017

JPM AWATAKA VIONGOZI KUWAENZI WATANGULIZI WAO…

Jengo la Amani na Usalama lililopo Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa nchini Ethiopia, limetangazwa rasmi kuwa litaitwa Mwalimu Julius Nyerere.

Jengo hilo limepewa jina hilo rasmi katika hafla iliyofanyika jana na kuhudhuriwa na Rais Dkt. John Magufuli pamoja na marais mbalimbali wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika,
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, mawaziri na mabalozi mbalimbali wanaohudhuria Mkutano wa 28 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika unaoendelea nchini Ethiopia.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, Rais Magufuli amewashukuru viongozi wote wa AU kwa kuamua jengo hilo liitwe jina la Mwalimu Julius Nyerere ikiwa ni kutambua mchango wake katika kupigania amani na usalama na amebainisha kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa Mwafrika halisi na kiongozi mahiri na shupavu.

0 comments:

Post a Comment