Monday 30 January 2017

DAR, LINDI NA MTWARA VINARA WA UKOMA TANZANIA..

Tanzania imeadhimisha Siku ya Ukoma Duniani tar 28 1 2017 ambapo mikoa ya Lindi, Morogoro, Dar es Salaam, Tanga na Mtwara imetajwa kuwa miongoni mwa mikoa 11 yenye idadi kubwa ya wagonjwa wa ukoma.


Taarifa iliyotolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Ummy Mwalimu, imezitaja halmashauri za wilaya zinazoongoza katika mikoa hiyo kuwa ni Lindi (Lindi Manispaa, Liwale, Lindi na Ruangwa), Morogoro (Halmashauri ya Ulanga, Kilombero na Mvomero), Dar es Salaam (Manispaa ya Temeke na Kigamboni), Tanga ( Halmashauri za Muheza, Mkinga  na Pangani).

Nyingine ni Mtwara (Halmashauri ya Nanyumbu na Newala), Rukwa (Halmashauri ya Nkasi), Pwani (Halmashauri ya Rufiji na Mkuranga), Geita (Halmashauri ya mji Geita na Halmashauri ya Chato), Tabora (Halmashauri ya Sikonge), Mwanza (Halmashauri ya Kwimba na Misungwi), na Ruvuma (Halmashauri ya Songea na Namtumbo).


Takwimu zinatuonyesha kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kutokomeza ugonjwa huu  kutoka kiwango cha utokomezaji cha watu 0.9  kati ya watu 10,000 mwaka 2006 na kufikia kiwango cha watu 0.4 kati ya watu 10,000 mwaka 2015 wakati kiwango cha kimataifa cha utokomezaji ukoma kinatakiwa  kuwa chini ya mgonjwa 1 katika watu 10,000.

0 comments:

Post a Comment