Tuesday 24 January 2017

LISSU: WAPINZANI TUSINYOOSHEANE VIDOLE

Mwanasheria Mkuu wa Chadema  Tundu Lissu, amesema kuwa matokeo ya uchaguzi mdogo wa ubunge na kata 20 si kielelezo cha Ukawa kushindwa katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020.

Lissu amesema kuwa kushindwa katika uchaguzi huo kunatokana na udogo au uchache wa maeneo yanayogombaniwa ambayo yanawapa fursa CCM kutumia nguvu kubwa za rasilimali za kidola ikilinganishwa na upinzani.
Amesema matokeo ya juzi si ya kushangaza kwani kata ya Duru ilikuwa ya kwao na wameitetea, zingine zote zilizopigwa zilikuwa za CCM.
“Hatujanyang’anywa iliyokuwa yetu tumeichukuwa,hatujanyakua zilizokuwa za kwao,hata hivyo funzo kubwa zaidi ya chaguzi hizi ni kwamba licha ya kupigwa kwenye chaguzi ndogo hizi,tumeendelea kufanya vizuri zaidi katika Uchaguzi Mkuu uliofuatia kipigo cha chaguzi hizi ndogo,tutumie mafundisho haya kujipanga vizuri zaidi kwaajili ya 2020,”amesema Lissu.
Chaguzi hizo ndogo za marudio zilimalizika juzi huku CCM ikijinyakulia kata 19 kati ya ishirini zilizokuwa zikigombaniwa Tanzania bara na Chadema kuambulia kata moja ya Duru.

Hata hivyo Lissu amesema kuwa wapinzani hawatakiwi kunyosheana vidole kwa kushindwa chaguzi hizo ndogo, bali wanatakiwa kurekebisha makosa na kasoro walizoziona katika uchaguzi huo.

0 comments:

Post a Comment