Shabiki
mmoja wa Arsenal alifanikiwa kumshawishi mkewe wampe mtoto wao jina la Arsenal
bila mwanamke huyo kugundua hilo.
Ilikuwa ni baada ya miaka miwili
ambapo mwanamke huyo Clare Smith, alijulishwa ujanja ambao mumewe alikuwa
ametumia.
Bi Smith kutoka eneo la Black town
jimno la New South Wales nchini Australia, alifichua hayo kwenye barua
aliyoandikia jarida moja, ambapo amesema mwenyewe hakugundua hilo hadi mumewe
alipomwambia.
Amesema waliamua kumwita binti
yao Lanesra, kwa sababu lilikuwa jina la kipekee na la kupendeza.
Lakini
bint yao alipotimiza umri wa miaka miwili, ndipo mume wangu akanifichulia
kwamba lilikuwa jina la Arsenal ukiandika kutoka nyuma.
0 comments:
Post a Comment