Serikali wilayani Geita
Mkoa wa Geita, imepiga marufuku walimu kuvaa mavazi yasiyolingana na
taaluma
yao, na upakaji wanja na rangi ya mdomo kupita kiasi wanapokuwa kazini.
Ofisa Utumishi wa
Wilaya ya Geita Thabitha Bugema, alitoa amri hiyo juzi wakati akizungumza na
walimu wakuu wa shule za msingi na waratibu elimu, kwenye kikao cha muongozo wa
kutumia fedha za elimu bure zilizotolewa na Serikali.
Bugema amesema
baadhi ya walimu wanavaa mavazi ya upotoshaji ambayo hayaendani na ya ofisini.
Amesema walimu wa
kiume huvaa suruali za jeans, fulana zenye nembo ya timu za mpira na wengine
kuvaa mlegezo na kunyoa nywele mitindo isiyo ya heshima.
Amesema kila
mtumishi wa Serikali anafahamu mavazi ya ofisini, na kuwataka walimu kubadilika
na kuvaa mavazi ya heshima yanayoendana na taaluma yao.
Ofisa Elimu Msingi
Wilaya ya Geita Deus Seif, amesema wamepokea Sh80 milioni kwa ajili ya elimu
bure na kuwataka wakuu wa shule kuhakikisha zinatumika kama ilivyopangwa.
Mkuu wa wilaya hiyo
Manzie Mangochie amewataka walimu na waratibu elimu, kufanya mikutano ya wazazi
ya kuwaelimisha maana ya elimu bure na kuwaeleza mambo ambayo Serikali inafanya
na wajibu wa wazazi kwa watoto wao.
0 comments:
Post a Comment