Kundi la RA ambalo ni la Kikristo nchini Ghana, linatarajia kuzindua kmtandao wa kijamii ambao unatajwa kuwa mtakatifu kinyume na uliozoeleka wa Facebook.
Mtandao huo mtakatifu inasemekana
utakuwa huru na usioegemea upande wa dini ya Kikristo hata chembe.
Kundi hilo la RA lenye jina LoveRealm, limesema kwamba mitandao ya kijamii
imejaa picha zenye maudhui ya utupu na ukatili.
Lakini kundi hilo limejinasibu kuwa
mtandao wao ujao, utawasaidia wale ambao walikuwa na mahangaiko ya kulinda imani
zao dhidi ya mitandao isiyokuwa na maadili, na mtandao huo utasaidia washirika
wake kutubu dhambi miongoni mwao.
Kwa sasa mtandao huo mtakatifu umekwisha
waalika maelfu ya wafuatiliaji Wakristo, wafanye majaribio ya kushiriki katika
tovuti hiyo katika kituo cha Pentekoste katika mji mkuu Accra.
0 comments:
Post a Comment