Tuesday 26 January 2016

TWIGA ALBINO APATIKANA TANZANIA..!!

Mwanasayansi Dk Derek Lee amegundua twiga albino kwenye hifadhi ya mbuga ya Tarangire,iliyopo katika Mkoa wa Arusha nchini Tanzania.

Mtafiti huyo alipiga picha mbalimbali zikiwa zinamwonyesha mnyama huyo akiwa katika kundi kubwa la twiga, huku akiwa na rangi ya kipekee ikilinganishwa na twiga wengine duniani.
Dk Lee alimgundua twiga huyo wakati akifanya utafiti kwenye mbuga hiyo, na nyingine za wanyama za barani Afrika.
Taarifa iliyoripotiwa na shirika la habari nchini Uingereza kupitia gazeti la Dailymail zimeeleza kuwa, twiga huyo adimu kupatikana duniani iwapo atahifadhiwa atakuwa kivutio cha pekee katika mbuga hiyo.
Twiga huyo anayejulikana kitaalamu kwa jina la ‘Omo’ likimaanishwa twiga mweupe/mwenye ulemavu wa ngozi ‘albino’, alionekana akizunguka katika mbuga hiyo katikati ya twiga wengine.
Dk Lee ambaye pia ni mtaalamu wa viumbe na mwanzilishi na mwanasayansi kutoka Wild Nature Instute, alimnasa twiga huyo katika kamera yake wakati akifanya uchunguzi huo kuhusu wanyama.

AMEsema uwezekano wa twiga huyo kukua kwa sasa ni mkubwa, lakini bado wanyama wakubwa wamekuwa wakimwinda na binadamu kwa ajili ya nyama za porini, na huenda rangi aliyonayo inaweza kumfanya yeye kuwindwa zaidi.

0 comments:

Post a Comment