Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape
Nnauye, amesema kuanzia
mkutano wa 11 wa bunge la jamuhuri ya muungano wa
Tanzania, Television ya taifa TBC
haitaonyesha matangazo ya moja kwa moja kwa muda wote wa vikao.
Waziri Nape amesema hayo leo Bungeni mjini Dodoma alipokuwa
akitoa taarifa ya serikali, na kusema kuwa matukio muhimu ya vikao vya bunge yatakuwa
yakirekodiwa na kurushwa katika kipindi maalum usiku katika kituo hicho.
Amesema sababu ya serikali kufanya hivyo ni
kupunguza gharama kubwa za uendeshaji, katika kurusha matangazo hayo ya moja
kwa moja.
Bonyeza play hapa chini kumsikia Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauy akieleza zaidi.
Bonyeza play hapa chini kumsikia Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauy akieleza zaidi.
0 comments:
Post a Comment