Kama wewe ni kati wale ambao wanakwepa kuoga wakitegemea mtelezo
wa Perfume,sikiliza hiii stori tokea
huko nchini Uingereza.
Ni kwamba kijana mmoja Thomas Townsend mwenye umri wa miaka 16,
amefariki dunia na uchunguzi unaonesha kuwa, kilichosababisha kifo chake ni
matumizi makubwa ya spray za manukato mwilini.
Kijana huyo Thomas alikutwa akiwa amepoteza fahamu chumbani kwake,na baada ya
upekuzi wa Polisi walikuta ndani ya chumba chake kuna makopo 42 ya manukato.
Na imeelezwa kuwa ile harufu yenye gesi kwenye manukato hayo,inatajwa
kuhusika kusababisha kifo chake.
Mama yake amesimulia
pia kwamba mtoto wake hakupenda kuoga, na alikuwa anaweza kupulizia nusu kopo
la manukato kwa wakati mmoja..!!
Mtaalam
mmoja wa masuala ya afya amesema kijana huyo Thomas,kafariki kutokana na
kuvuta hewa ya gesi ya butane inayowekwa kwenye manukato...!!
0 comments:
Post a Comment