Kanda
ya video ya CCTV, imetolewa ambapo daktari mmoja nchini Urusi alimpiga ngumi
mgonjwa na kumuua.
Kisa hicho kilitokea katika mji
wa Belgorod kilomita 670 kusini mwa mji mkuu wa Moscow, mnamo mwezi Disemba
tarehe 29 2015.
Mgonjwa huyo alikuwa amempiga
teke muuguzi mmoja,kabla ya daktari huyo kumpiga ngumi ya kichwa kulingana na
vyombo vya habari vya Urusi na kuzirai kabla ya kuaga dunia akiwa hospitalini.
Wachunguzi wanadhani kwamba
hakumuua kwa makusudi, lakini wameanzisha kesi ya uhalifu.
Habari hiyo ilisambaa baada ya
kanda hiyo kutolewa.
0 comments:
Post a Comment