Licha
ya kuhusishwa na uchafu na mazingira duni, kunguni ameibuka kuwa mdudu mwenye
uwezo mkubwa wa kustahimili hatari dhidi ya maisha yake.
Utafiti mpya umebaini kuwa wadudu
hao wanaweza kustahimili sio tu tanuri ya moto na baridi kali, bali pia madawa
ya kisasa ya kuua wadudu wanaotambaa.
Kunguni wamegundulika kuwa
wanaweza kustahimili kupuliziwa dawa nyingi ya sumu kwa kuimarisha uwezo wake
wa kujikinga dhidi ya sumu moja baada ya nyengine.
Wadudu hao ambao huishi kwa
kufyonza damu ya wenyeji wake wakiwa usingizini, wanauwezo mkubwa wa
kibayolojia ya kujikinga dhidi ya sumu kali.
Hii ni kusema kuwa kadri vizazi
vya kunguni vinavyopuliziwa madawa yenye sumu, ndivyo wadudu hao
wanavyoimarisha uwezo wake wakuzuia maafa miongoni mwa watoto wao.
Aidha watafiti wanaema kuwa
vipimo 1000 vya sumu kali aina ya (neo-nicotinoid) vinahitajika kuua kunguni
mmoja huko Marekani, katika majimbo ya Cincinnati na Michigan ikilinganishwa na
maeneo mengine duniani.
Watafiti hao sasa wanasema kuwa kuna hatari kubwa ya
mdudu huyo kuenea kote duniani, kutokana na utandawazi na soko huria ambao
umefanya ulimwengu kuwa kitongoji kikubwa.
Aidha wanasayansi hao wanashauri
kutafutwa mbinu tofauti na mpya ya kukabiliana na kunguni pasi na kutumia sumu,
kama vile kutafuta wadudu wengine wanaoweza kuwala ilikuzuia wadudu hao kuenea
kote duniani.
Taarifa hiyo imechapishwa katika
jarida la utabibu la The Journal of Medical of Entomology.
0 comments:
Post a Comment