Tuesday, 5 January 2016

Wagundua tiba ya Ukimwi..!

Wakati dunia ikiwa na zaidi ya watu 34 milioni wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU), madaktari nchini Hispania wametangaza kugundua tiba ya ugonjwa huo wanayodai ni uhakika.

Kwa kutumia damu ya kupandikiza kutoka kwenye kitovu mwana (umbilical cord) cha mtu ambaye ana vinasaba ambavyo havipokei virusi hivyo vya Ukimwi, wataalamu hao wa tiba wa Hispania wanaamini kuwa wanaweza kutibu ugonjwa huo baada ya mafanikio waliyopata kwa mgonjwa mmoja.
Madaktari hao wa Kitengo cha Taifa cha Upandikizaji (ONT) cha Hispania, walichukua damu ya vitovu mwana vya watu wenye vinasaba ambavyo havipokei VVU na kuipandikiza kwa mtu anayeishi na virusi hivyo.
Baada ya miezi mitatu mgonjwa huyo alipimwa na kuonekana hana virusi.
Daktari wa Programu ya Upandikizaji kutoka Taasisi ya Tiba ya Catalan Barcelona Rafael Duarte, amesema mgonjwa aliyetibiwa kwa njia hiyo Timothy Brown (37), alikuwa anaishi na VVU tangu mwaka 2009, na madaktari hao walithibitisha kuwa amepona baada ya kupandikizwa damu hiyo.
Mgonjwa mwingine aliyefanyiwa majaribio ya tiba hiyo alipona VVU, lakini miaka mitatu baadaye alifariki kwa ugonjwa wa saratani.
Timu ya madaktari wa Hispania ililiambia gazeti la kila siku nchini humo la El Mundo kuwa wana uhakika kuwa wameleta mapinduzi katika mapambano ya Ukimwi na magonjwa yanayofanana na hayo.

Dk Duarte amesema mwaka 2015 umekuwa wa kujivunia ugunduzi huo mkubwa duniani, ingawa alitahadharisha kuwa tiba kamili haiwezi kupatikana katika siku za usoni.

0 comments:

Post a Comment