Choo
cha kisasa ambacho kina uwezo wa kujifungua unapokaribia na pia kujiosha, ni
moja ya vitu vinavyoonyeshwa katika maonyesho ya kimataifa ya teknolojia mpya
za bidhaa za elektroniki Las Vegas.
Choo hicho kilichopewa jina
Neorest, pia humsafisha anayekitumia kwa kifaa kinachotoa maji moto na hewa mtu
akiwa ameketi,pia kina teknolojia inayokiwezesha kuua bakteria na virusi.
Kampuni ya Toto iliyotengeneza choo hicho, imesema muundo
huo wa sasa bado unaendelea kuboreshwa.
Choo hicho hata hivyo si kwamba kitakuondolea kabisa
majukumu yote ya usafi chooni, kwani hakiwezi kujiosha upande wa nje iwapo
kutakuwa na uchafu.
Maonyesho hayo ambayo kwa
Kiingereza yanajulikana kama Consumer Electronics Show hufanyika kila mwaka
ambapo kampuni mbalimbali na wavumbuzi huonyesha teknolojia za karibuni zaidi.
0 comments:
Post a Comment