Mashirika ya
kutetea haki za binaadamu nchini Afrika Kusini, yanasema yamekasirishwa na
mpango wa
kuwapa ufadhili wa elimu ya vyuo vikuu wasichana 16 ikiwa watabakia
bikira.
Wasichana
kutoka wilaya ya Uthukela ya mkoa wa mashariki wa KwaZulu-Natal, wana fursa ya
kupewa msaada wa elimu wa hadi miaka mitatu, ili kugharamia masomo yao katika
chuo kikuu.
Meya wa eneo
hilo Jabulani Mkhonza amesema kuwa, wasichana wanaishi katika hatari kubwa ya
kunyanyaswa, kupata mimba na hata kuambukizwa virusi hatari vya Ukimwi.
Lakini
wapinzani wanasema mpango huo ni wa kuwadunisha wanawake, wakiongeza kuwa pesa
za walipakodi hazipaswi kutumiwa kukiuka haki za wasichana.
0 comments:
Post a Comment