Watu
zaidi ya 50 wamefariki nchini Taiwan, kutokana na wimbi la baridi kali ambalo
limeathiri maeneo ya Asia Mashariki.
Watalii zaidi ya elfu 60 pia
wamekwama Korea Kusini, kutokana na karidi hiyo.
Vyombo vya habari nchini Taiwan
vinasema kuwa, vifo hivyo vimetokana na kushuka sana kwa kiwango cha joto
mwilini na wengine wakafariki kutokana na maradhi ya moyo.
Hii ni baada ya viwango vya joto
kushuka ghafla wikendi.
Hayo yakijiri theluji nyingi
imesababisha kufungwa kwa uwanja wa ndege katika kisiwa cha Jeju nchini Korea
Kusini, ambacho ni maarufu sana kwa watalii.
Wimbi hilo la baridi limeathiri
sana Hong Kong, Uchina kusini na Japan.
Walioathirika zaidi Taiwan ni wazee wanaoishi maeneo ya
kaskazini kama vile Taipei, Kaohsiung na Taoyuan.
Katika baadhi ya maeneo ya Taiwan
viwango vya joto vilishuka hadi nyuzi 4C siku ya Jumapili.
Hong Kong hali ilikuwa mbaya
zaidi, baadhi ya maeneo yakishuhudia vipimo vya joto vya nyuzi 3C, kikiwa
ndicho kiwango cha chini zaidi kushuhudiwa eneo hilo katika kipindi cha miaka
60.
0 comments:
Post a Comment