Shirika
la kimataifa la kutetea haki za bimaadamu Amnesty International, linasema nchi
ya Misri
inasumbuliwa na suala la mgogoro wa haki za kibinadamu kwa kiwango
kikubwa,na haya ni matokeo ya miaka mitano baada ya maandamano yaliyomn'goa
raisi Hosni Mubarak.
Kikundi kimoja cha cha kampeni
kinasema kuwa siku za hivi karibuni kuwa,idara ya usalama imeamua kuvamia
nyumba zipatazo elfu tano mjini Cairo ili kuwabaini watu waliopanga njama za
kuandamana hii leo katika kumbukumbu ya kung'olewa kwa Mubarak.
Shirika la Amnesty linasema jeshi
la Polisi la taifa hilo la Misri linakiuka wajibu wake, kwa kuwakamata
wanaharakati wengi au kuwafanya wengi kujificha ili kupiga marufuku maandamano
hayo kufanyika.
0 comments:
Post a Comment