Monday 25 January 2016

TETEMEKO LA ARDHI MELILLA…

Watu katika eneo la Uhispania kaskazini mwa bara la Afrika la Melilla, walilazimika kukimbilia
mitaani baada ya tetemeko la ardhi  la ukubwa wa  6.3 kipimo cha Richter,lililoyaharibu majengo yakiwemo makao makuu ya  serikali.
Rais wa serikali ya Melilla ambayo ni milki ya Uhispania Juan Jose Imroda, amesema hakuna hasara ya binaadamu ilioripotiwa.
Televisheni ya Uhispania ilionyesha picha za majengo yalioporomoka na watu wakikimbia mitaani, wengine wakiwa bado wamevaa nguo za kulalia.

Melilla yenye wakaazi elfu 85 imezungukwa na Morocco na bahari ya Mediterania.

0 comments:

Post a Comment