Wednesday 27 January 2016

BARIDI KALI YASABABISHA SHULE KUFUNGWA…

Jimbo lenye wakazi wengi zaidi nchini Pakistan la Punjab, limeamuru kufungwa
  kwa shule zote kwa siku tano na kuwataka wanafunzi wapatao milioni 22.5 kubakia nyumbani.
Hatua hiyo haihusiani na hofu ya usalama baada ya watu wenye silaha kukishambulia chuo kikuu nchini humo, bali ni kutokana na hali mbaya ya baridi kali.
Waziri wa elimu wa jimbo hilo Rana Mash hood, amesema idadi kubwa ya wanafunzi wanapatwa na mafua na kichomi katika kipindi cha baridi  kali.
Hii ni kutokana na nyuzi joto hushuka na kufikia nyuzi joto 4 katika mji mkuu  Lahore, na ukosefu  mkubwa wa gesi husababisha  shule kushindwa kuweka  mazingira ya joto.

Waziri huyo ameliambia shirika la habari la reuters kwamba, siku mbili  ilizopita wazazi walilalamika juu ya hali mbaya ya hewa, pamoja na magonjwa kwa watoto wao.

0 comments:

Post a Comment