Makao
makuu ya kanisa katoliki mjini Vatican yamefichua maelezo kuhusu kitabu kipya
cha papa
Francis "the name of God is Mercy" jina la Mungu ni rehema,
kitakachochapishwa kote duniani kwa muda wa siku mbili zijazo.
Maandishi ya kitabu hicho
yanatokana na mahojiano kati ya papa na mwanahabari, ambapo anaangazia mada ya
rehema, na umuhimu wa kuwa na rehema kwa watu waliotengwa katika jamii.
Papa pia anaangazia jinsi ambavyo
huwa anaomba msamaha wakati wa kutubu.
0 comments:
Post a Comment