Mji
mmoja kaskazini mwa Italia, unasherehekea kuzaliwa kwa mtoto wa kwanza tangu
mapema miaka ya 1980.
Meya wa mji wa Ostana ulioko eneo
lenye vilima la Piedmont, anasema kuzaliwa kwa mtoto huyo ni kutimia kwa ndoto
ya jamii ndogo inayoishi katika mji huo.
Idadi ya watu katika mji huo
imeshuka sana katika kipindi cha miaka 100 iliyopita, na walikuwa wamesalia
watu 84 pekee na ni nusu yao pekee huishi katika mji huo bila kuhamahama Gazeti
la La Tampa linasema.
Mtoto Pablo aliyezaliwa katika
hospitali moja mjini Turin,amefikisha idadi ya watu mjini humo hadi 85 sasa.
Meya Giacomo Lombardo anasema mji
wa Ostana ulikuwa na watu 1,000 mapema miaka ya 1900, lakini wakaanza kupungua
baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia.
Amesema watu walipungua zaidi
kuanzia 1975 ambapo ni watoto 17 pekee waliozaliwa kati ya 1976 na 1987, ambapo
mtoto wa mwisho mvulana alizaliwa.
Tangu wakati huo hakuna mtoto
mwingine aliyezaliwa hadi sasa mji huo ulipompokea Pablo.
Mji huo unajaribu kukabiliana na
hali ya kushuka kwa idadi ya watu, kwa kuunda nafasi za kazi.
Wazazi wa Pablo Silvia na Jose
walikuwa wamepanga kuhamia ng’ambo miaka mitano iliyopita, lakini ripoti
zinasema waliamua kukaa baada ya kupewa kazi.
Sherehe kubwa imeandaliwa mjini
Ostana kusherehekea kuzaliwa kwa Pablo, na kwa mujibu wa La Stampa sanamu ya
korongo imewekwa kwenye lango la kuingia mji kwa heshima yake.
0 comments:
Post a Comment