Shirika
la habari la Al Jazeera limefunga matangazo ya Televisheni nchini Marekani
ikiwa ni chini ya miaka mitatu tangu kuzindua huduma zake nchini humo.
Al Jazeera imesema kuwa
imelazimika kufunga matangazo yake kutokana na ugumu wa mazingira ya soko la
televisheni nchini humo.
Shirika hilo lenye makao makuu yake Qatar limesema kuwa
badala yake linaimarisha na kupanua huduma ya kimtandao katika maeneo ambayo
yanaendesha mfumo huo kwa sasa.
Taarifa zinasema kuwa Al Jazeera imeshindwa kuwavutia
watazamaji wa kutosha nchini Marekani ili kuweza kujitengenezea faida.
0 comments:
Post a Comment