Waziri wa Fedha mpya wa Afrika Kusini, Malusi Gigaba, amesema wakati
umefika wa kubadilisha sana uchumi.
Amesema, kwa muda
mrefu Afrika Kusini inahodhiwa na wawekezaji wa nchi za nje.
Pia amekiri kwamba
kutolewa kazini kwa waziri aliyemtangulia hapo jana, Pravin Gordhan, kumeigawa
nchi.
Bwana Gordhan
anayeheshimiwa kimataifa, alipotolewa kazini ghafla, katika mabadiliko ya
baraza la mawaziri aliyofanya Rais Jacob Zuma, kulizuka malalamiko kutoka kwa
watu wengi, pamoja na makamu wa rais, Cyril Ramaphosa, na wanasiasa mashuhuri
katika chama tawala cha ANC.
Vyama vya upinzani,
vinasema, Bwana Gordhan aliondolewa, kwa sababu alimzuwia Rais Zuma na
washirika wake, wasipate nafasi ya kufikia mali ya taifa.
0 comments:
Post a Comment