Wanasayansi wanasema
kwa mara ya kwanza wamegundua kuna unyevu unaoizunguka sayari ilio kama dunia.
Wameichunguza sayari hii inayotambulika
kama GJ 1132b ambayo ukubwa wake ni zaidi ya dunia kwa mara 1.4 na iko umbali
wa miaka 39 ya kasi ya muanga.
Uchunguzi wao
unaonyesha kuwa sayari hii imezingirwa na gesi ya methane au maji au
mchanganyiko wa zote mbili.
Habari hii ni
muhimu sana kwa kuendeleza masomo yanayohusiana na maisha nje ya mfumo wa jua.
Hata hivyo kuna uwezekano kuwa mtu hawezi kuishi katika dunia hii kwa sababu ya
joto jingi la 370C.
Dkt. John
Southworth ni mtafiti mkuu kutoka chuo kikuu cha Keele na anasema:
"Kulingana na maarifa niliyo nayo, joto la juu zaidi ambalo mwanadamu
ameweza kustahimili hapa duniani ni 120C."
Kugunduliwa kwa
sayari ya GJ 1132b kulitangazwa kwanza mwaka wa 2015. Sayari hii iko katika
mkusanyiko wa Vela, anga ya kusini.
Ingawa ukubwa
wake ni sawa na dunia, nyota inayozunguka ni ndogo na yenye mwanga mdogo kuliko
jua.
Wakitumia
darubini huko Chile, watafiti hao waliweza kuisoma sayari kwa kutazama jinsi
ilizuia mwanga wa nyota nyingine zilizopita mbele yake.
Watafiti
wanasema kuwa ni vigumu kwa kitu choochote chenye uhai kuishi katika sayari ya
GJ 1132b.
Dkt. Southworth
anasema, " Tulicho onyesha ni kuwa kuna nyota ambazo zinaweza kuwa na anga
na kwa vile dunia au nyota kama hizi ni nyingi, kuna uwezekano kuwa moja kati
zao zinaweza kuwa na uhai."
0 comments:
Post a Comment