Mwanamume mmoja raia wa Australia
ambaye alikuwa na bili kubwa ya kulipa baada ya kupata mlo kwenye mkahawa mmoja
aliruka na kuingia baharini ili kukwepa kulipa bili hiyo.
Polisi walimfuata kwa kasi
mwanamuziki hiyo ambaya baadaye alisema kuwa alikimbia kumsaidia rafiki yake
kujifungua mtoto katika fukwe za bahari.
Alikuwa na bili ya zaidi ya dola
450.
Terry Peck ambaye amefunguliwa
mashtaka ya wizi baadaye alidai kuwa chakula hicho hakikua kimepikwa kwa njia
inayotakikana.
Mwanamuziki huyo mwenye umri wa
miaka 33 alifikishwa mahakani leo Jumatatu baada ya kisa hicho kilichotokea
katika mgahawa wa Omeros Bros.
Australia si nchi pekee ambapo kuna
visa vya wateja kula kwenye mikahawa na kukosa kulipa.
Mwezi uliopita polisi wa Uhispania
walimkamata mtu anayeshukiwa kuwa kiongozi wa genge ambalo lilikuwa na tabia ya
kula kwenye mikahawa na kisha kutoroka kaskazini mwa nchi.
Kundi hilo liliwajumuisha watu 100
lilikula chakula cha thamnia ya euro 22 katika mkahawa wa Bembibre's El Carmen
mwezi Machi na baadaye wote wakakimbia bila kulipa.
0 comments:
Post a Comment