Aliyekuwa Waziri wa
Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Jimbo la
Mtama, Nape Nnauye amemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dkt. John
Magufuli kuunda tume huru ya kuchunguza matukio ya uhalifu, utekaji na uvamizi
yanayoendelea hapa nchini.
Ameyasema hayo
alipokuwa akiongea na wananchi Jimboni kwake Mtama, amesema kuwa kutokana na
matukio ya kihalifu yanavyoongezeka kuna haja kubwa ya kuunda tume hiyo huru
ili kuweza kuchunguza na kubaini wahusika.
Amesema kuwa haiwezekani
vikundi hivyo vya uhalifu vikawa na nguvu zaidi kushinda vyombo vya dola hapa
nchini na kusababisha hofu kubwa kwa wananchi.
“Ombi langu kwa Rais
Dkt. Magufuli namuomba aunde tume huru ichunguze matendo haya yasijirudie tena
kwa sababu yasipochukuliwa hatua yataharibu sura ya Tanzania pia yataweza
kuibuka makundi ya wahuni kuanza kuteka watu hovyo,”amesema Nape.
Aidha Mbunge huyo
amesema watu wanaofanya mambo hayo wanalengo la kuwagombanisha wananchi na
Serikali yao jambo ambalo sio zuri kwa taifa.
Hata hivyo, amesema
kuwa mpaka sasa haamini yule mtu aliyemtolea silaha siku ya mkutano wake na
waandishi wa habari kama alitumwa na hajui vyombo vya Ulinzi na Usalama
vinafanya nini mpaka sasa.
0 comments:
Post a Comment