Kutokana na tatizo la upungufu wa
walimu katika Shule ya Msingi Mbalawala Manispaa ya Dodoma,
wazazi wa watoto
wanaosoma shuleni hapo wamewazuia watoto wao kwenda shule kuanzia leo hadi hapo
watakapopelekewa walimu wa kutosha.
Wazazi hao walichukua uamuzi huo
katika mkutano wa kijiji na kamati ya shule hiyo, uliofanyika shuleni hapo
mwishoni mwa wiki.
Shule hiyo ina walimu watano tu
wanaohudumia mikondo saba.
Wakizungumza katika mkutano huo wazazi
hao walisema kuwa, wameamua kuchukua uamuzi huo kwa kuhofia watoto wao kupata
mimba za utotoni kutokana na kukosa uangalizi wa walimu wakiwa shuleni.
Mkazi wa kijiji hicho Hamis Sanda amesema
shule hiyo ya muda mrefu ina walimu wachache, na kila mara wamekuwa wakiahidiwa
kupelekewa walimu, lakini hakuna utekelezaji unaofanyika hali inayosababisha
wanafunzi kushindwa kusoma.
Alisema wamechoshwa kuona watoto wao
wakienda shule lakini hawajui chochote kutokana na kutofundishwa na wengi wao
waliopo darasa la saba, hawajui kusoma wala kuandika.
0 comments:
Post a Comment