Rais wa Marekani Donald Trump ameadhimisha siku mia moja uongozini kwa
kutoa hotuba ya kushambulia wanahabari na kutetea mafanikio yake.
Bwana Trump
amewaaambia wafuasi wake huko Pennsylvania kwamba ameridhika kuwa pamoja nao
badala ya kuhudhuria dhifa ya chakula cha jioni na wanahabari ama
'Correspondents diner' iliyokuwa ikifanyika katika ikulu ya White House wakati
huo.
Hafla hiyo ni miongoni
mwa hafla maarufu sana mjini Washington.
Akihutubia umati
mkubwa katika jimbo la Pennsylvania, Rais Trump amelinganisha na kutofautisha,
kile ametaja 'siku mia moja za wanahabari kushindwa na kazi yao', na mafanikio
yake ambapo amesema amekuwa akitimiza 'ahadi zake kila siku', hususan kurejesha
kazi za viwanda na kumaliza mzozo katika sekta ya makaa ya mawe.
Pennsylvania ni jimbo
linalotegemea uchumi wa uchimbaji madini, na lilikuwa muhimu sana katika
uchaguzi wa mwaka jana.
Awali maelfu ya watu
waliandamana nchini Marekani dhidi ya utawala wa rais Trump na msimamo wake
kuhusu mazingira.
0 comments:
Post a Comment