Manuwari za Uchina zimewasili Ufilipino kwa mara ya kwanza baada ya miaka
saba huku Ufilipino ikiimarisha uhusiano wake na Uchina.
Manuwari hizo tatu
zilitia nanga mjini Davao.
Ziara hiyo inafanywa siku
moja baada ya mkutano wa nchi za Kusini Mashariki mwa Asia, ambao ulifanywa
Ufilipino ambapo malalamiko dhidi ya harakati za Uchini katika Bahari ya Kusini
ya Uchina, hazikuzungumzwa sana.
Kabla ya Rodrigo
Duterte kuwa rais wa Ufilipino, nchi hiyo ikilalamika vikali juu ya hatua za
Uchina katika bahari hiyo.
0 comments:
Post a Comment