Ziara ya Waziri Mkuu wa Ethiopia hapa nchini imetoa changamoto
kubwa kwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), baada ya Rais wa Jamhuri ya
Muungano kuliagiza Shirika hilo kuweka mikakati madhubuti ya kuzalisha na kuuza
umeme kwa bei nafuu.
Rais
Dkt. Magufuli ametoa agizo hilo Jijini Dar es salaam wakati wa mazungumzo na
Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Desalegn ambaye yuko hapa nchini kwa ziara
ya kikazi ya siku mbili, amesema kuwa Waziri Mkuu wa Ethiopia ameahidi kuipatia
Tanzania umeme megawati 400 kwa ajili ya kusambaza nchini.
Aidha,
Desalegn amesema kuwa atatoa ofa ya megawati 400 kwa ajiri ya kusambaza nchi
nzima, kwani Ethiopia umeme unauzwa kwa bei ndogo ya senti sita, hali ambayo
ilipelekea kwaRais Magufuli kuliagiza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco)
kujifunza kile ambacho Ethiopia inafanya ili waweze kuzalisha umeme wa bei
nafuu.
“Hii itakuwa ni hatua nyingine ya
Tanesco kujifunza namna Ethiopia wanavyozalisha umeme na kuuza kwa bei nafuu na
wao waanze kufanya hivyo,”amesema Rais Magufuli.
Hata hivyo, katika hatua nyingine
Rais Magufuli amesema kuwa Waziri Mkuu wa Ethiopia ameahidi kufungua ubalozi
hapa nchini na kuahidi kumpa eneo Mjini Dodoma.
0 comments:
Post a Comment