Sunday 9 April 2017

VIDEO: HAYA NDIYO MANENO YA ROMA BAADA YA KUPATIKANA.


Msanii wa muziki wa hip hop Roma Mkatoliki, Moni pamoja na wenzao 2 wameachiwa na jeshi la polisi baada ya kuhojiwa na kufanyiwa vipimo.

Wasanii hao walitekwa na watu wasiojulikana Alhamisi hii wakiwa Tongwe Record na mapema Jumamosi hii walionekana wakiwa oysterbay polisi.
Akiongea na waandishi wa habari akiwa Mwananyamala hospitali muda mchache baada ya kufanyiwa vipimo na kuachiwa huru, Roma alisema kwa sasa anaendelea vizuri pamoja na wenzake.

0 comments:

Post a Comment