Takriban watu13
wameuwa kwenye mlipuko uliotokea katika kanisa moja kaskazni mwa Misri.
Mlipuko huo ulilenga
kanisa la St George's Coptic, lililo mji wa Tanta huko Nile Delta.
Vituo kadha vya
runinga vilisema kuwa takriban watu 40 walijeruhiwa.
Chanzo ya mlipuko huo
bado hakijulikani lakini jamii ya wakiristo wachache nchini Misri wamekuwa
wikilengwa na wanamgambo wenye itikadi kali.
Mwezi Disemba mwaka
uliopita, watu 25 waliuawa wakati bomu lilipolipuka katika kanisa la Coptic
cathedral mjini Cairo wakati wa sala.
Ghasia dhidi ya
wakiristo wa Coptic, zimekuwa nyingi miaka ya hivi karibuni, hasa tangu mwaka
2013 wakati jeshi lilipompindua rais aliyekuwa amechaguliwa.
Baadhi ya wafuasi wa
rais aliyetimuliwa Mohammed Morsi, ambaye alitoka kundi la Muslim Brotherhood,
waliwalaumu wakiristo kwa kuunga mkono kupinduliwa kwake.
0 comments:
Post a Comment