Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza
linamshikilia Samweli Masumbuko (32), Mkazi wa Kata ya Mahina wilayani
Nyamagana, kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa darasa la pili (jina
linahifadhiwa) mwenye
umri wa miaka 10.
Kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi, mtuhumiwa
huyo alikamatwa Aprili 1, mwaka huu saa 11:00 jioni katika Mtaa wa Mwembeni,Kata
ya Mahina.
Kamanda Msangi alisema
mtuhumiwa anadaiwa kuwa alimbaka mwanafunzi huyo Machi 25, mwaka huu saa 11:00
jioni, lakini kwa kipindi chote hicho hakuweza kusema kwa mtu yeyote hadi
Aprili 1, mwaka huu mama yake alipogundua mwanawe kufanyiwa ukatili huo.
Alisema upelelezi dhidi ya
watu waliohusika kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha au kushawishi
ukatili huo bado unaendelea na kwamba mtuhumiwa anahojiwa na Jeshi la Polisi na
pindi uchunguzi utakapokamilika atafikishwa mahakamani.
0 comments:
Post a Comment