Hofu kubwa inazidi kutanda
kwa baadhi ya vigogo na viongozi wa umma juu ya mpango mpya ulioanzishwa na
Serikali wa kuhakiki mali zao.
Aidha, hofu hiyo inatokana na uwekaji wa
mfumo mpya Serikalini wa kufuatilia taarifa za kweli za mali za viongozi wa
umma na kutunzwa vizuri kupitia mifumo ya kielektroniki.
Utekelezaji wa mpango huo wa uboreshaji
wa taarifa za mali za viongozi wa umma, ndio unaowapa hofu viongozi na vigogo
hao kwa sababu unawaweka katika wakati mgumu wale wenye tabia ya kuficha ukweli
kuhusu mali wanazomiliki.
Hivi karibuni Ofisi ya Rais Sekretarieti
ya Maadili ya Viongozi wa Umma inayojihusisha na utunzaji wa na
ufuatiliaji juu ya taarifa zinazowasilishwa na na viongozi wa umma, imeunda
mfumo wa kielektroniki wa menejimenti ya taarifa za kimaadili.
Hata hivyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angella Kairuki amesema kuwa mfumo huo mpya utarahisisha upatikanaji wa taarifa bora na kwa wakati
Hata hivyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angella Kairuki amesema kuwa mfumo huo mpya utarahisisha upatikanaji wa taarifa bora na kwa wakati
0 comments:
Post a Comment