Takriban watu 20 wameuawa na wengine kujeruhwia kwenye
madhababu yaliyo mji wa Sargoda, mkoa wa Punjab nchini Pakistan.
Naibu kamishna wa
polisi Liaquat Ali Chatta, alisema kuwa mshukiwa mkuu ni mhudumu wa madhabu
hayo Abdul Waheed.
Manusura mmoja
aliwaambia polisi kuwa bwana Waheed aliwaita wafuasi katika chumba chake mmoja
baada ya mwingine, na kuwapa chakula kilichokuwa na sumu.
Yeye na wenzake kisha
waliwaua watu hao kwa kuwapiga wakitumia vifaa.
Kisa hicho kilifichuliwa
na mwanamke aliyekuwa amejeruhiwa katika hospitali iliyo karibu, ambaye alikuwa
amefanikiwa kutoroka.
Kisha polisi
walifululiza kuenda eneo hilo na kumkamta bwana Waheed pamoja na watu wengine
ambao wanaaminiwa kuwa washirika wake.
Sababu ya mauaji hayo
haijulikani lakini polisi wanasema kuwa mshukiwa huyo alionekana kuwa na
matatizo ya kiakili.
Abdula Waheed mweye
umri wa miaka 50, amekiri kuwaua watu hao, kwa sababu alihofu kuwa walikuwa
wameenda kumuua, kwa mujibu wa AFP
0 comments:
Post a Comment