Sheria mpya zitaanza kutekelezwa katika jimbo la magharibi mwa Uchina la
Xinjiang, ambako utawala wa Beijing unaaendeleza kile wanachokisema ni kuzuia
ueneaji wa itikadi kali.
Miongoni mwa hatua
wanazochukua ni kupiga marufuku mavazi ya wanawake ya niqab au burka ya kuziba
uso au kufuga ndevu ndefu kwa wanaume wa jamii ya waislamu wa Uighurs.
Kumekuwa na visa vya
makabiliano makali ya mara kwa mara baina ya maafisa polisi na wakaazi wa jimbo
hilo la Uighurs, linalotaka kuwa na mamlaka na uhuru zaidi.
Wapinzani wa sheria
hizo wanasema zinalenga kukandamiza utamaduni wa jamii ya waislamu wa wa
Uighurs huko Uchina.
0 comments:
Post a Comment