Watu waliojihami na bunduki wamempiga
risasi na kumjeruhi mwanamazingira na mwandishi mzoefu mzaliwa wa Italia, Kuki
Gallmann.
Amepigwa risasi ya tumbo akiwa kwenye shamba lake kaunti ya
Laikipia.
Mwezi uliopita makahawa wake wa kifahari uliteketezwa na watu
wanaoshukiwa kuwa wafugaji.
Bi Gallmann, amekuwa mwenyeji wa Kenya tangu miaka ya sabini, na
anafahamika zaidi kutokana na kitabu chake 'I Dreamed of Africa'.
Filamu ya kitabu hicho pia ilitolewa, mhusika mkuu, akiwa mwigizaji
maarufu wa Marekani ,Kim Basinger.
0 comments:
Post a Comment