Sunday 23 April 2017

UFARANSA NAMCHAGUA RAIS MPYA..

 
Raia wa Ufaransa wanapiga kura ya urais hivi leo.
Kwa mara ya kwanza baada ya miongo kadhaa , huu umekuwa uchaguzi usiotabirika.

Takriban asilimia 30 ya wapiga kura wanaaminika kwamba hawajatangaza msimamo wao.
Wawaniaji watatu wakuu hawana historia yoyote ya kisiasa akiwemo Emmanuel Macron, Marine le Pen na Jean-Luc Melenchon
Wagombea maarufu (Kushoto kuenda kulia): François Fillon, Benoît Hamon, Marine Le Pen, Emmanuel Macron na Jean-Luc Mélenchon
Mpinzani wao mhafidhina Francois Fillon, amehudumia serikali katika nyadhfa kadhaa za uwaziri katika kipindi cha miongo miwili.
Hakuna yeyote anayetarajiwa kuibuka na ushindi katika duru ya kwanza, na wawili watakaoongoza uchaguzi huo watamenyana na katika duru ya pili mwezi ujao.

Usalama umeimarishwa kufuatia shambulizi la kigaidi lililotokea katikati mwa mji mkuu Paris alhamis, ambapo afisa mmoja wa polisi aliuwawa.

0 comments:

Post a Comment