Wataalamu wa Saikolojia kutoka
Chuo Kikuu cha Penn State Marekani, wamegundua jambo ambalo linawashangaza
wengi katika swala la malezi kwa watoto.
Katika utafiti wao wamesema
kuwa zaidi ya 90% ya watoto waliopitia maisha ya kunyanyaswa, kupigwa au
kudhalilishwa kingono, wanapevuka haraka ukilinganisha na watoto wanaolelewa
kwa upendo.
Professor Jennie Noll aliliambia Jarida la Adolescent
Health kuwa, watoto
hasa wa kike hupevuka kabla ya muda, pia watoto wa aina hii huota matiti mapema
ukilinganisha na watoto wa kawaida.
Akielezea uhusiano ulipo baina ya mtoto
kunyanyaswa na kupevuka kabla ya wakati, Dr Noll amesema watoto wanaokuwa
katika mazingira kama hayo huzalisha homoni nyingi zinazotokana na msongo
mkubwa wa mawazo, hivyo kuharakisha muda wa kupevuka.
Wanasaikolojia hao pia
wamesema mtoto anayenyanyaswa yuko hatarini zaidi kupata saratani ya ovary na
matiti, ukilinganisha na watoto ambao hulelewa kwenye mazingira ya upendo na
amani.
0 comments:
Post a Comment