Msanii kutoka
Ufaransa Abraham Poincheval anaendelea kutamia mayai ya kuku akiwa na matumaini
kwamba mwishowe yataangua vifaranga.
Msanii huyo anatumia
joto kutoka kwa mwili wake kutamia mayao hayo 10.
Poincheval ambaye
hufanya uigizaji wa kuigiza mambo ya ucheshi lakini ya hatari, tayari ameishi
wiki mbili ndani ya dubu, miongoni mwa mambo mengine ya kushangaza.
Atakuwa katika chumba
maalum ambacho anatamia mayai, ambapo watalii wanaweza kumtazama katka makumbusho
ya Palais de Tokyo mjini Paris.
Anatarajia kutamia
mayai hayo kwa siku 21 hadi 26.
"Kusema mweli,
kimsingi, ni kama nimekuwa kuku," anasema.
Poincheval, 44,
ameuita uigizaji huo wake - "Oeuf" (Yai kwa Kifaransa).
Badala ya kutamia
mayai hayo kwa kuchutuma juu yake moja kwa moja, anatumia kiti maalum ambacho
kina mfuko eneo lake la kukalia. Hapo ndipo mayai hayo yamewekwa.
Poincheval atakuwa amejifunga
blanketi kuzuia joto kupotea.
Aidha, anapanga kula
vyakula vinavyoongeza sana joto mwiliki, kama vile tangawizi.
Wakati wa haja,
atatumia kijisanduku kidogo kilichomo mvunguni mwa kiti chake.
Ndipo mayai hayo
yaangue vifaranga, hahitaji kuondoka zaidi ya dakika 30 kwa siku. Anapanga
kutumia muda huo kula chakula.
Uigizaji wa sasa wa
Poincheval anaufanya baada ya uigizaji wake aliouita "Pierre" (Jiwe
kwa Kifaransa), ambapo aliishi ndani ya jiwe kubwa lililokuwa limechongwa
sehemu ya kutoshea mwili wake ndani.
0 comments:
Post a Comment