Friday 29 May 2015

Wachina 15 mbaroni kwa kugushi....!!



 Raia 15 wa China wamefunguliwa mashitaka nchini Marekani kwa tuhuma za udanganyifu wa matokeo na nyaraka za kitaaluma walizozitumia kujiunga na elimu ya juu nchini Marekani.
Kwa mjibu wa waendesha mashtaka nchini humo,wamebaini kuwa vijana hao wa China wamekuwa fanya udanganyifu wa kutumia simu wakati wa majaribio ya kujiunga na vyuo hivyo.
 Idara ya sheria nchini Marekani imesema kuwa kwa kipindi cha minne iliyopita wamekuwa wakikwepa mfumo halali wa uchaguzi wa majina ya chuo na badala yake kutumia majina bandia na pasi za kusafiria.
Iwapo watakutwa na hatia kutokana na tuhuma hizo,raia hao wa China watafungwa hadi miaka 20 jela.

0 comments:

Post a Comment