Friday 29 May 2015

Malori toka Tanzania yasababisha ajali 227 Zambia………….



Wakati Serikali na wadau wa usafiri wakiendelea kutafuta mwarobaini wa ajali nchini, imeelezwa kuwa malori ya Tanzania yamesababisha ajali 227 nchini Zambia kati ya Januari na Mei.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwenye Gazeti la Lusaka Times la Zambia, imeelezwa kuwa Tanzania inatakiwa kutafuta suluhisho la kudumu la kudhibiti ajali zinazosababishwa na malori ya Tanzania wanayokwenda nchini humo.
Likikariri ripoti iliyotolewa na Kikosi cha Usalama Barabarani cha Zambia mwezi huu, gazeti hilo limesema katika ajali hizo 227, ajali 37 zilipoteza maisha ya watu 42.
Ripoti hiyo ilitaja sababu kubwa ya ajali hizo kuwa ni mwendo kasi, vizuizi barabarani, uchovu wa safari ambao umekuwa ukisababisha baadhi ya madereva kuegesha malori yao vibaya na kusababisha madhara kwa watumiaji wengine wa barabara.

0 comments:

Post a Comment