Thursday 14 May 2015

Kichanga cha siku tatu chatupwa……….



Mtoto mchanga wa kiume wa siku tatu katika mtaa wa Masanga Wilaya ya Igunga, ameokotwa akiwa amekatwa viungo vyake na watu wasiojulikana.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Masanga Julius Kitundu, amesema mtoto huyo aliokotwa na wasamaria wema pembezoni mwa barabara ya lami.
Mwenyekiti huyo ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na kuwaomba watoe ushirikiano kwa jeshi la Polisi katika kuwasaka wahusika.
Baadhi ya wananchi wamelaani kitendo hicho cha kinyama,na kusema wataanzisha msako mkali ili kuhakikisha waliohusika wanakamatwa na mama aliyejifungua anashikiliwa.

0 comments:

Post a Comment